
Mhudumu
wa kike aliyegeukia uandishi wa habari amefichua mkasa wake mbaya mno
wa miezi 15 akiwa ameshikiliwa mateka na magaidi wa Kisomali ambako
watekaji hao walimbaka na kucheza kamari ya Kirusi huku wakiwa na
bunduki kubwa ya mashambulizi.
Amanda
Lindhout alikwenda kishamba kwenye taifa hilo fukara na fukivu mwaka
2008 akiwa na umri wa miaka 24 baada ya kumshawishi rafiki yake wa kiume
wa zamani kuambatana naye kwenye matembezi hayo ya hatari.
Amanda na Nigel Brennan, mpigapicha wa Australia mwenye miaka 36, walitekwa nyara katika siku yao ya tatu nchini humo.
Mwandishi
mmoja wa Somalia, Abdifatah Mohammed Elmi, ambaye alikuwa akifanya kazi
kama mkalimani wao, pia alikamatwa, lakini akaachiwa baada ya miezi
kadhaa.
Miezi
15 ya wapenzi hao katika mateka inaelezewa katika taarifa zao zote za
kutisha kwenye kitabu cha Amanda, 'A House in the Sky', kitakachoingia
sokoni wiki ijayo, kwa mujibu wa gazeti la the New York Post.
Brennan
hakuwa na uzoefu katika ukanda wa vita na Amanda alitumia muda kidogo
nchini Irak ambako aliwahi kushikiliwa mateka wakati fulani kabla.
Huko
Mogadishu, aliwatisha waandishi wakongwe kwa ujasiri wake na ushamba
ambao Robert Draper alimtumia baruapepe rafiki yake wa kike: "Anaelekea
kujiingiza au mtu mwingine kuuawa."
Somalia,
ambayo imekosa serikali kuu kwa miaka 18, ni sehemu hatari kwa
wafanyakazi wa kimataifa wa kujitolea na waandishi wa habari
wakikabiliwa na hatari kutekwa na kushikiliwa na watu wenye silaha hadi
watakapolipiwa kiasi cha fedha kwa ajili ya kuwakomboa.
Utawala
wa upande wa Magharibi unaoongozwa na Rais Hassan Sheikh Mohamud
unapambana na al Shabaab na makundi mengine ya waasi, na unashikilia
pungufu ya miraba michache ya mji mkuu.
Amanda na Brennan walichukuliwa mateka baada ya magaidi kunyatia hoteli yao.
Walitekwa nyara Agosti 23, 2008 wakati walipokwenda kutembelea kambi ya wakimbizi nje ya mji mkuu huo.
Walielezwa kwamba Dola za Marekani milioni 3 za fedha za fidia zinahitajika kwa wote.
Masharti hayo haraka yakawa mabaya kufuatia kupigwa na kunyimwa chakula na Amanda kubakwa na kundi la wanaume kwa zamu.
Wakihofia kwamba wanaweza kuuawa, wawili hao wakaamua kwamba fursa yao ya kupona itaimarika kama watasilimu na kuwa Waislamu.
Haraka wakatenganishwa na kuwekwa kwenye vyumba tofauti ambako mateso yakaendelea.
Nigel hakuwa na msaada wakati alipokuwa akisikia Amanda akibakwa kupitia kwenye kuta nyembamba za gereza lao.
Mmoja
wa watekaji aliweka bunduki yake kubwa ya mashambulizi kwenye kichwa
cha Amanda na kucheza kamari ya Kirusi, liliripoti the Post.
Mara kwa mara walihamishiwa kwenye nyumba tofauti tofauti ambako waliwapa majina tofauti.
Wawili
hao waliishi katika hofu kubwa kwamba wangekabidhiwa kwa waasi wasio na
huruma wa al Shabaab, ambao Marekani inadai ni tawi la al Qaeda nchini
Somalia.
Amanda
akapatwa na maambukizi ya minyoo kwenye uso wake, nywele zake na kucha
za vidole vya miguuni wakati Nigel alipata ugonjwa wa kuhara damu.
Baada
ya siku 100, Amanda alichukuliwa peke yake kwenda kwenye jangwa.
Alielezwa kupiga magoti na kichwa chake kikibanwa nyuma kwa mvuto mkali
wa nywele zake, kisu kilisukumwa dhidi ya koo lake.
Aliomba asiuawe na kupewa simu ya mkononi kuongea na mama yake na kuahidi mamilioni ya dola ama sivyo atauawa.
Anaandika,
kwa mujibu wa the Post: "Nilitupwa kwenye uchafu, nikilia kama mnyama,
kama kitu fulani kilichojeruhiwa na kutoweza kuzungumza."
Wawili
hao waliopagawa walichora mpango wa kutoroka baada ya Amanda kuwa
amepelekwa kwenye jangwa peke yake usiku mmoja na kulazimishwa kuomba
asiuawe kwenye uchafu.
Walitoroka
kupitia dirisha la bafuni na kuruka urefu wa futi 12 hadi chini na
kutimua mbio huku wakipiga mayowe kwenye msikiti moja wa mahali hapo
kuomba msaada.
Wananchi
wa mahali hapo hawakuwa na uwezo wa kuwaokoa wawili hao kutoka kwa
watekaji wao ambao walikuwa jirani nyuma yao, washikiliaji mateka hatari
zaidi waliokuwa na bunduki kubwa ya maashambulizi.
Mtu
mmoja katika msikiti huo alijaribu kumkabili Amanda akiwa na bunduki
lakini hakuweza kufyatua risasi. Mwanamke huyo alimkumbatia Nigel kwa
karibu kabisa.
Mateka
hao wakapigwa kabla ya kuchukuliwa na kupelekwa kwenye nyumba ambako
vyumba vilikuwa kama selo nyeusi na panya wakikimbizana ndani yake.
Walielekezewa bastola na kufungwa minyororo baada ya jaribio lao la
kutoroka.
Kumekuwa
na madai kwamba Amanda amejifungua mtoto wa kiume aliyempa jina la
Osama wakati akiwa mateka lakini hakuzungumzia hilo," limeripoti the
Post.
Mwishowe,
waliachiwa huru Novemba 2009 baada ya siku 460 wakiwa mateka baada ya
familia zao kukusanya pamoja maelfu ya dola na kutetea maisha yao.
Muda mfupi baada ya kuachiwa kwake, alisema: "Nilipigwa na kuteswa. Ulikuwa wakati mgumu, kupita kiasi."
Nigel
alichapisha kitabu cha 'Price of a Life' mwaka 2011 wakati kitabu cha
Amanda kitakuwa sokoni wiki hii. Wapenzi hao wa zamani kwa sasa
hawawasiliani tena.
Amanda pia alianzisha taasisi yake ya Global Enrichment Foundation wakati akiwasaidia wanawake nchini Kenya na Somalia.
No comments:
Post a Comment